Psalms 90:1-6
(Zaburi 90–106)
Umilele Wa Mungu Na Udhaifu Wa Mwanadamu
(Maombi Ya Musa, Mtu Wa Mungu)
1 a Bwana, wewe umekuwa makao yetu
katika vizazi vyote.
2 bKabla ya kuzaliwa milima
au hujaumba dunia na ulimwengu,
wewe ni Mungu tangu milele hata milele.
3 cHuwarudisha watu mavumbini,
ukisema, “Rudini mavumbini, enyi wanadamu.”
4 dKwa maana kwako miaka elfu
ni kama siku moja iliyokwisha pita,
au kama kesha la usiku.
5 eUnawatowesha wanadamu katika usingizi wa kifo,
nao ni kama majani machanga ya asubuhi:
6 fingawa asubuhi yanachipua,
ifikapo jioni huwa yamenyauka na kukauka.
Copyright information for
SwhKC