Psalms 90:1-6

(Zaburi 90–106)

Umilele Wa Mungu Na Udhaifu Wa Mwanadamu

(Maombi Ya Musa, Mtu Wa Mungu)


1 a Bwana, wewe umekuwa makao yetu
katika vizazi vyote.

2 bKabla ya kuzaliwa milima
au hujaumba dunia na ulimwengu,
wewe ni Mungu tangu milele hata milele.


3 cHuwarudisha watu mavumbini,
ukisema, “Rudini mavumbini, enyi wanadamu.”

4 dKwa maana kwako miaka elfu
ni kama siku moja iliyokwisha pita,
au kama kesha la usiku.

5 eUnawatowesha wanadamu katika usingizi wa kifo,
nao ni kama majani machanga ya asubuhi:

6 fingawa asubuhi yanachipua,
ifikapo jioni huwa yamenyauka na kukauka.

Copyright information for SwhKC